BUSTANI

Responsive Advertisement

FAHAMU ZAO LA KUNDE NA UZALISHAJI WAKE







 UTANGULIZI
Kunde ni zao ambalo linaweza kulimwa kwa ajili
ya chakula na bishara ni zoa lenye kiasi
kukubwa cha protini na majani yake yanaweza
kutumika kama mboga za majani.Ni zao ambalo
linatoa mavuno ya Kiasi cha kilogram 500 hadi
1500 kwa ekari.

HALI YA HEWA IFAAYO
Ni zao linalostahimili ukame, Kunde hukubali
vizuri katika mwinuko wa mita 0 hadi 1500
kutoka usawa wa bahari.kunde huweza kulimwa
katika maeneo yapatayo mvua kidogo kiasi cha
milimita 500 hadi 1200 kwa mwaka.Hukuwa
vizuri katika joto la nyuzi 28 had 32 C

ARDHI IFAAYO KWA KILIMO CHA KUNDE

Huweza kulimwa katika udongo usiotuamisha
maji wa aina tofauti tofauti kuanzia kichanga
hadi mfinyazi.Zinaweza kupandwa katika
udongo usio na rutuba ya kutosha lakini hustawi
vizuri katika udongo wa tifutifu kichanga au
tifutifu mfinyanzi au  mchanganyiko wa mfinyazi
na kichanga wenye p.H kati ya 6 hadi 7, ni vizuri kupima udongo kwa ajili ya uhakika zaidi

MAANDALIZI YA SHAMBA LA KUPANDA KUNDE


Shamba la kunde liandaliwe mapema kabla
shughuli ya upandaji kuanza, Kama ni la kukata
miti mikubwa miti ikatwe mapema,Kama ni la
kufyeka nyasi na miti midogo shughuli hii
ifanyike mapema kabla hatua ya kulimwa kwa
shamba kwa kutumia trekta,Pawatilla,jembe la
ng'ombe au la mikono.shamba lisawazishwe na
kukusanywa mabaki ya mimea au visiki na
mawe madogomadogo kama yapo.

MBEGU BORA ZA KUNDE

Kuna aina mbalimbali za mbegu bora za kunde
ambazo zimegawanyika katika makundi
makubwa mawili.Kunde zinazosimama na kunde
zinazotambaa.

BAADHI YA MBEGU BORA NA SIFA ZAKE
1.TUMAINI
Hukomaa kwa muda wa siku 75 – 90. Aina hii ya
kunde husambaa ina maua yenye rangi za
zambarau na mbegu zake ni mviringo. Maeneo
yanayoshauriwa kupanda ni yenye mwinuko wa
mita 0 – 1500 toka usawa wa bahari. Inahitaji
udongo mwepesi wenye rutuba na usiotuamisha
maji. Kunde hizi hutoa mazao hadi tani 3
(kilogram 600 - 1500 kwa ekari)kwa hekta moja.
Huvumilia virusi vya mozaiki vinavyotokana na
wadudu mafuta wa kunde na bakteria. Aina hii
ya kunde ilizalishwa mwaka 1992 na Kituoa cha
Utafiti cha Ilonga kwa ushirikiano na Naliendele.

  2.FAHARI
Aina hii hukomaa kwa siku kati ya 75 – 90.
Mmea husambaa na maua yana rangi ya
zambarau. Mbegu zake ni za mviringo. Hustawi
maeneo yenye mwinuko wa mita 0 – 1500
kutoka usawa wa bahari. Hutoa hadi tani 3 kwa
hekta moja (kilogram 600 - 1500 kwa ekari ).
Huvumilia magonjwa ya CABMV na mabaka.
Fahari ilitolewa mwaka 1982 na Kituo cha Utafiti
Ilonga kwa kushirikiana na Naliendele

  3.VULI_1
Inakomaa kwa siku 55 – 65. Hukua ka kunyooka
na kusambaa kidogo. Mbegu zake ni nyekundu
na za mviringo. Inastawi vizuri maeneo yenye
mwinuko wa mita 0 – 1500 toka usawa wa
bahari. Ikipataiwa matunzo mazuri huto hadi tani
2 kwa hekta moja (Kilogram 450-800 kwa ekari).
Vuli – 1 inavumilia CABMV, BP na BB Vuli – 1
ilizalishwa mwaka 1987 kutoka kituo cha utafiti
Ilonga.

4.VULI_2
Inakomaa baada ya siku 65 – 70 baada ya
kupandwa inaota ikiwa imenyooka na kusambaa
kidogo. Mbegu zake zina weupe uliofifia na ni
mviringo. Aina hii husitawi vizuri maeneo yenye
mwinuko wa mita 0 – 1500 kutoka usawa wa
bahari. Katika matunzo mazuri aina hii huzalisha
hadi tani 3.5 kwa hekta moja(Kilogram 800
-1200 kwa ekari) . Vuli – 2 huvumilia CABMV, BP
na BB Vuli – 2 ilizalishwa mwaka 1987 kutoka
kituo cha utafiti Ilonga.


KUPANDA KUNDE

Kunde hupandwa mwishoni mwa msimu wa
mvua ili kuziepusha kukauka wakati mvua
inaendelea kunyesha.na pia unweza kupanda
wakati zao jingine linakaribia kuvunwa au katika
shamba lilivunwampunga na lina unyevu wa
kutosha.Muda mzuri wa kupanda kunde ni
akuanzia mwezi Februari mwishoni hadi Machi
na Aprili kwa maeneo ambayo mvua huchelewa
kuisha.
  KUMBUKA; Mbegu zinazotambaa za
kunde zipandwe miezi miwili kabla ya mvua
kuisha kwani hizi huchukua siku nyingi kukomaa
na Mbegu zinazosimama zipandwe mwezi
mmoja kabla ya mvua kuisha.
Kunde huitaji kiasi cha kilogram 4-12 za mbegu
kwa ekari.kiasi cha mbegu kitategemea ukubwa
wa mbegu,(mbegu kubwa zitahitajika kilogram
nyingi) nafasi za upandaji,Ukipanda karibu
karibu na mbegu itahitajika nyingi,Ubora wa
mbegu katika uhotaji.Zisizoota vizuri huitaji
mbegu nyingi zaidi


NAFASI YA UPANDAJI

Unaweza kutumia nafasi zifuatazo kwa kupanda
kunde zako
KUNDE ZINASOSIMAMA-Tumia sentimeta 45
hadi 50 mstari hadi msatari na sentimeta 15 hadi
20 shina hadi shina katika mstari / Sm
 ( 50 X20 )

KUNDE ZINAZOSAMBAA-
Tumia nafasi ya Sentimeta 70 hadi 75 mstari hadi mstari Kwa sentimeta 25 hadi 30 shina hadi shina katika mstari / Sm ( 75 X 30 )
Panda kwa kufikia kiasi cha sentimeta 2.5 hadi 5
ardhini na tumia mbegu tatu kwa kila shimo na
baadaye punguza uache 2 kwa kila shimo kama
unauhakika wa mbegu zako unaweza kupanda
moja kwa moja mbili mbili kwa shimo

PALIZI NA KUPUNGUZA MIMEA      KATIKAMISTARI

Palilia na Punguza mimea mapema katika
shamba lako la kunde.ili ikuwe ikiwa na afya
bora.

MBOLEA YA SAMADI NA MBOLEA ZA VIWANDANI

Kama shamba lako halina rutuba ya kutosha
unaweza kuongeza samadi kiasi cha tani tano
kwa ekari moja na uhakikishe mbolea hii
imemwagiwa au imenyeshewa na mvua ya
kutosha kuiozesha kabla ya kupanda kunde
zako na pia unaweza kupanda kwa kutumia
mbolea ya TSP kiasi cha Kg 50 kwa ekari na
baadaye kukuzia mbolea ya SA kiasi cha Kg 50
kwa ekari.

WADUDU NA MAGONJWA KUNDE
KUDHIBITI WADUDU WAHARIBIFU WA KUNDE

Wadudu waharibifu wa zao la Kunde wako katika
makundi mawili:-
     1. Kundi la kwanza ni la wadudu
wanaoshambulia mimea ikiwa shambani.
 Inamaana mmea hushambuliwa baada ya kuona
hali inapokomaa na kutoa mbegu. Kundi la
wadudu hawa lina tabia ya kufyonza (Sap =
supu) ya mmea kwenye majani, matawi,
mashina, maua hata mbegu hasa zikiwa changa
kama vitunda. Njia hii ndiyo pekee kwa wadudu
wa kundi hili kujipatia mlo ili waishi na
kuzaliana. Katika kundi la pili kuna wadudu
wenye tabia ya kukata mashina na kuangusha
mimea michanga na wengine hutafuna majani
na maua. Zaidi ya uharibifu katika kula mimea,
wadudu wengi ni hifadhi ya viini vya magonjwa
ya virusi.

 2.Kundi la pili ni la wadudu waharibifu baada
ya mavuno kuwekwa ghalani.
 Athari ya wadudu hawa inapelekea wakulima kupoteza chakula
ghalani pia kupunguza chakula ghalani pia
kupunguza ubora wa mazao yanapopelekwa
sokoni mfano Mahindi yanapofunguliwa soko
lake ni duni. Jamii za wadudu na athari zao
zinaelezwa katika aya zifuatazo:-

1. KUNDE:
(ii) Foliage beetle (Ootherca mutabilis)
Wadudu hawa hushambulia mimea ya kunde
baada ya mbegu kuota (Seedling stage). Wakiwa
kwenye hatua ya mdudu kamili (adult stage)
hushambulia majani kwa kula sehemu kati ya
vihimili vya majani (area between leaf veins).
Mashambulizi ya wadudu wengi husababisha
mmea kupoteza majani yote na hatimaye mmea
kufa.
Kuzuia jamii ya wadudu hawa:
Dawa za chemikali aina ya endosulfan, Karate
n.k. huagamiza mashambulizi kwa mpulizo
mmoja.
(i) Aphids (Aphis gaccivora)
Hawa ni kati ya wadudu wenye kusababisha
hasara kubwa katika zao la kunde.
Wanapendelea kula mvunga wa majani (under
leaf), sehemu za vishina na hata vitumba (pools)
vya mbegu. Athari za mashambulizi: Mmea
hudumaa, majani husinyaa na kukunjamana pia
hupukutika kabla hayajazeeka hatimaye mmea
hufa.
Kuzuia Aphids: Dawa za kemikali aina ya
phosphomiolon na dimethoate kwa cc 40 katika
lita 10 za maji.
(ii) Flower thrips (Megalurothrips sjostedti)
Hatua ya mdudu kamili hushambulia maua.
Mimea ikishambuliwa sana haizai matunda
kwasababu maua yameharibika. Mashambulizi
yakiwa makubwa zao lote huangamia.
Kuzuia: Kwa kutumia chemikali aina ya
Cypermethrin – kiwango cha cc 40 katika lita 10
za maji.
(iii) Podborers (Maruca testulalis)
Wadudu hawa hula mvungu wa majani, ganda la
shina na vitumba vya mbegu katika hatua ya
kukomaa. Athari: Mmea hudumaa, umbo la
majani huharibika (olistorted leaves) na
hupukutika kabla ya kuzeeka. Mimea mingi hasa
michanga hufa.
Uzuiaji: Kwa kutumia chemikali aina ya
phosphomidon na dimethoate kwa kiwango cha
cc 40 katika lita 10 za maji.
(iv) Podsucking bugs (Anoplemenia,dentires,
Acanthomia SPP)
Wadudu hawa hushambulia mikunde katika
hatua ya kuweka vitumba (pods). Hasara,
inayosababishwa, na wadudu hawa hufikia 90%.
Madhara makubwa huletwa na hatua ya wadudu
kamili (adult stage/ kwa kufyonza “Sap = Supu”
ya vitumba teketeke ambavyo husinyaa na
kukauka bila kukomaa wala kuwa na mbegu.
Kuzuia: Kwa kutumia chemikali za Endosulfan au
dimethoate kwa kiwango cha cc 40 katika lita 10
za maji.
(v) Cowpea storage weevils (Callosobrunchus
macuhates callosobrun ams chinensis).
www.kilimofaida.blogspot.com
Mashambulizi ya wadudu hawa wawili huanzia
shambani wakati kunde zimekaribia kukomaa.
Wadudu hutaga mayai kwenye vitumba
vilivyokomaa. Mayai yakiangauliwa, funza
hupenya kupitia kwenye matobo
yanayosababishwa na wadudu wengine. Funza
wakianguliwa hushambulia mbegu na uharibifu
hufikia 70% ya mbegu safi.
Kuzuia: Tumia chemikali aina ya Acteric Super
Dust 100 mg za unga wa dawa katika 10 Kg za
mbegu safi (Seed grain)


NAMNA YA KUZUIA MAGONJWA YA ZAO LA

KUNDE:

Magonjwa hatari yanasababishwa na vimelea
vya virusi na vya bacteria aina tabia na uzuiaji
wa magonjwa haya ni kama ifuatavyo:-

(i) Cowper aphid-born mosaic virus
Ugonjwa huu husababishwa na virusi na
hupelekea mkulima kupata hasara ya 13 – 87%
ya zao.
Dalili za ugonjwa huu ni michirizi ya
rangi ya kijani iliyochanganyika na njano au ya
ugoro (mosaic & mottling) kwenye majani.
Kuzuia: Kwa kutumia aina za kunde zenye
kustamili ugonjwa huu kama Tumaini, Fahari na
Vuli.

(ii) Bacterial blight (Xanthomonus vignicola)
Ugonjwa huu hushambulia sana miche na kiasi
cha 60% ya miche yote hufa.
Dalili: Majani,vitumba au mashina ya mimea
iliyoathirika huwa na vidonda vyenye rangi kati
ya njano ya chungwa. Katika mashambulizi
makubwa vidonda vidogo huungana (merge –
coleasce) na eneo kubwa la majani huharibika.
Ugonjwa hushamiri katika kipindi cha mvua
nyingi (Kifuku) na umwagiliaji kwa juu (Overhead
irrigation).
Kuzuia: Tumia mbegu zinazovumilia ugonjwa
kama Tumaini, Fahari na Vuli.

(iii) Bacterial blight (Xanthomonas Spp)
Ugonjwa hushambulia aina ya kunde pori na
zinazolimwa.
Dalili: Vidonda vidogo huonekana uvunguni mwa
majani. Katika mimea dhaifu (more susceptible)
vidonda huungana na kuwa na umbo la duara
lenye ukubwa wa: kipenyo cha 1-3 cm.
Mwanzoni vidonda huonekana kufutuka
mvunguni mwa jani kadiri vinapokomaa huwa
na rangi ya kahawia upande wa juu na majani.
Baada ya muda vidonda hukauka na hubakisha
migonyeo sehemu zilizoathirika. Majani mengi
yaliyathirika hubadilika kuwa njano na baadaye
huanguka / hupukutika.
Ueneaji: Ugonjwa huenea kwa kasi wakati wa
kifuku (mvua nyingi) na umwagiliaji unapokuwa
wa juu. (overhead irrigation). Kimelea cha
bacteria huyu hudumu kwenye punje (mbegu).
Kwa hiyo mbegu za namna hii huota zikiwa na
viini vya ugonjwa.
Kuzuia: Kutumia mbegu zenye kustahimili
ugonjwa huu kama Tumaini, Fahari na Vuli

(iv)Powdery Mildew (Ukungu)
Dalili-Majani yanakuwa na vidoti vya njano
ambavyo vinabadilika kuwa vya kahawia au
kijivu haraka na ambapo kunakuwa na unga
unga katika majani.
Kinga na tiba-Panda mbegu zinazostahimili
ukungu,Pulizia dawa za ukungu (Fungicide).
anza kupuliza wiki tatu baada ya mimea kuota
na kuendelea kulingana na hali halisi ya
ugonjwa.

UVUNAJI

Vuna kunde zako baada ya kukomaa na kuanza
kukauka kwa kung'oa mashina au kuchuma kwa
mikono.Kisha zisambaze kunde zako au
mashina yako juani ili zikauke zaidi na uweze
kuziondoa kwa urahisi kutoka katika maganda
yake.
Unaweza kuondoa maganda yake kwa
mkono au kuupigapiga taratibu au kwa
kutwanga katika kinu taratibu bila kuzipasua
Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa simu namba 

Post a Comment

0 Comments